HISTORIA YA GWIJI WA POP MICHAEL JACKSON
Michael Joseph Jackson alizaliwa mnamo tarehe 29 Agosti mwaka 1958 huko Gary, Indiana Marekani na kufariki dunia mnamo tarehe 25 Juni 2009. Alikuwa mwimbaji, dansa na mburudishaji kutoka nchini Marekani. Hufahamika zaidi kwa jina la kiheshima au utani kama Mfalme wa Pop. Hutambulika kama mburudishaji aliyepata mafanikio zaidi kwa muda wote, na alikuwa ni mmoja kati ya waburudishaji wenye mvuto mkubwa kwa hadhira katika medani ya muziki. Michael ana mchango mkubwa katika soko la mziki duniani kote hasa katika dansi la jukwaani na pia alipenda kuanika hadharani maisha yake binafsi, imemfanya awe kioo cha ulimwengu katika tamaduni maarufu kwa ziaidi ya miongo minne .
Akiwa pamoja na ndugu zake, Michael
alianza mziki kwa mara ya kwanza akiwa kama mwanachama mdogo kabisa katika
kundi la The Jackson 5 mnamo mwaka wa 1964. Michael Jackson alianza kuonekana jukwaani akiwa na miaka
mitano tu pamoja na kaka na dada zake. Alitokea familia ya wanamuziki ya Jackson
Five. Kuhusu miaka yake ya awali
alisimulia mara kadhaa ya kwamba baba alimlazimisha kufanya mazoezi mno ya
kucheza na uimbaji hivyo Michael hakuufaidi kabisa utoto maana alikuwa
akihudhulia majukwaani akiwa na umri mdogo zaidi na kulazimishwa kuishi kama
mtu mzima na mashughuli akiwa na kundi lililokuwa likiratibiwa na baba
yao mzazi mzee Jackson.
Baada ya mafanikio makubwa ya kundi
hilo Michael alianza kujitegemea kama msanii binafsi mnamo mwaka 1971. Na albamu yake bora kabisa aliitoa mwaka 1982 na
kuipa jina la Thriller
imebaki kuwa albamu yenye mauzo bora kwa muda wote duniani. Staili ya muziki
wake, sauti na namna ya utumbuizaji wake
zilitambulika vizazi kwa vizazi na hata mavazi yake nayo yalivutia kwa rangi na
hata mishono yake ya kipekee.
Maisha binafsi ya Michael yalikuwa hayakaukiwi utata kwa miaka kadhaa moja ya utata huo ni kashifa za kujibadilisha kwa mwonekano wake hali hii ilianza kujidhihilisha mwishoni mwa miaka ya 1970 na kuendelea, Michael aliyezaliwa kwa maumbile ya Mwamerika mweusi mwishoni alikuwa na ngozi nyeupe usoni na baada ya upasuaji kadhaa pua yake ikawa nyembamba si pana tena. Mwenyewe alijitetea kwa kusema kwamba badiliko la rangi lilisababishwa na ugonjwa. Ingawa hoja hiyo ilikosa mashiko kwa wasikilizaji na wafuatiliaji wa maisha yake na kuendelea kusababisha maswali mengi hasa kwenye vyombo vya habari na mashabaki wake.
Mnamo mwaka wa 1993 Michael alishtakiwa kwa kosa la
udhalilishaji wa kijinsia kwa watoto, ingawa hakukutwa na hatia baada ya
uchunguzi kukamilika. Michael katika maisha yake amewahi kuoa mara mbili,
kwanza alioa mnamo 1994 na akaja kuoa tena mnamo 1996. Na alibahatika kupata watoto
watatu. Michael, alimwoa Bi. Lisa Marie Presley, binti wa Elvis
Presley. Jackson, pia alikuwa akimiliki
eneo kubwa lenye makazi lililoitwa Neverland, ambalo baadaye liliuzwa kwa
kampuni na nusu bado inamilikiwa na mwenyewe.
Michael alifariki mnamo tar. 25 Juni 2009 kwa kuzidisha
kiasi cha dawa za usingizi wakati anajiandaa na ziara ya tamasha lake la This Is It, ambalo
lilitakiwa lianze katikati ya mwaka wa 2009. Iliripotiwa kwamba alitumia dawa
aina ya propofol na lorazepam. Afisa uchunguzi wa vifo wa
wilaya ya Los Angeles lieleza baada ya uchunguzi kuwa kifo chake kilisababishwa
na daktari wake kutokuwa makini wakati akitoa dozi ya dawa kwa mteja wake na
iliaminika kuwa hali hiyo ni sawa na uuaji. Na mashtaka yalielekezwa kwa
daktari wake binafsi kwa kosa la kuua bila kukusudia. Kifo cha Jackson kilileta
huzuni kubwa ulimwenguni kote hasa kwa wadau na wapenzi wa mziki wa pop.
Mazishi yake yalitangazwa na kushirikisha watu wote duniani kote kwa njia mbali
mbali huku maelfu ya watu wakihudhuria katika kuuaga mwili wake.
Michael Jackson maisha yake yalikuwa
wazi sana na yaliwavutia wengi. Pia, alishawahi kukumbwa na kashfa ya kwa unyanyasaji wa mtoto, lakini hakukutwa na kosa. Alifanya upasuaji maalumu ili
abadilishe mwonekano wake. Watu waliomtazama hawakupatana kama mabadiliko ya
kimaumbile yalikuwa ama tokeo la kuona aibu kuonekana kama Mwafrika au jaribio
kuwa na uso linalorahisisha mawasiliano yake na watu wa bara zote.
Na Emmanuel Venance.
HISTORIA YA GWIJI WA POP MICHAEL JACKSON
Reviewed by Burudani Za Bongo
on
01:16
Rating:
Reviewed by Burudani Za Bongo
on
01:16
Rating:

No comments: